EU-BURUNDI-MASHAURIANO-SIASA-UCHUMI
EU kupunguza kiwango cha fedha kwa wanajeshi wa Burundi Somalia
Umoja wa Ulaya unapanga kupunguza ufadhili wake wa kifedha kwa wanajeshi wa Burundi wanaolinda amani nchini Somalia.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
EU inasema lengo la kufanya hivyo ni kumshinikiza rais Piere Nkurunziza kuja katika mazungumzo ya kisiasa na wapinzani na kumaliza mzozo unaoshuhudiwa nchini humo.
Burundi ina wanajeshi 5,400 nchini Somalia chini ya mwavuli wa AMISOM na kila mwaka Umoja wa Ulaya unatoa Dola Milioni 52 kuilipa serikali na wanajeshi.
Haitakuwa mara ya kwanza kwa Mataifa ya Magahribi kuondoa misaada yake kwa nchi ya Burundi tangu mvutano wa kisiasa nchini humo mwaka uliopita.