EgyptAir yatekwa nyara: abiria atishia kulipua mkanda wake
Ndege ya shirika la ndege la Misri EgyptAir iliyokuwa imebeba abiria 81 na wafanyakazi 7 ikifanya safari kati ya Alexandria na Cairo ambayo ilikua imetekwa nyara na watu wasiojulikana imetua katika mji wa Larnaca, nchini Cyprus.
Imechapishwa:
Taarifa hii ni kwa mujibu wa runinga ya serikali ya Cypus na mamlaka ya uwanja wa ndege wa Cairo.
BREAKING: Egypt officials say EgyptAir plane hijacked flying from Alexandria to Cairo, now headed to Cyprus
— The Associated Press (@AP) March 29, 2016
Kwa mujibu wa chanzo hicho, abiria wa Misri
Egyptian and Cypriot officials say a hijacked Egypt plane has landed in Cyprus; bomb on board suspected https://t.co/iex7rpLZ8Q
— The Associated Press (@AP) March 29, 2016
wanasadikiwa kuwa wameondolewa katika ndege hiyo mjini Larnaca.
Shirika la habari la Ufaransa la AFP limebaini kwamba abiria ametishia kulipua mkanda wake kwa mujibu wa vyanzo vya mamlaka ya usafiri wa anga.
Watekaji nyara waliwasiliana na maafisa mamalaka ya uwanja wa ndege saa 8:30 asubuhi saa za Cyprus (sawa na saa 5:30 asubuhi alfajiri saa za kimataifa) na ndege hiyo aina ya Boeing 737-800, ambayo ilikuwa ikifanya safari kati ya Alexandria na Cairo ilipewa kibali cha kutua saa 8:50 asubuhi, polisi imesema.
Negotiations with the Hijacker result in the release of all the passengers, except the crew and four foreigners.
— EGYPTAIR (@EGYPTAIR) March 29, 2016
Watekaji nyara hawajazungumza chochote na kikosi cha askari polisi kimetumwa katika uwanja wa ndege wa Larnaca.