Pata taarifa kuu
GBAGBO-ICC-IVORY COAST

Mawakili wa Gbagbo, wasema rais Ouattara aliingia madarakani kwa kutumia nguvu akisaidiwa na Ufaransa

Mawakili wa utetezi wa rais wa zamani wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo, wanamtuhumu rais wa sasa, Alassane Ouattara kwa kuchukua madaraka kwa nguvu akisaidiwa na taifa la magharibi lililowahi kuitawala nchi hiyo, Ufaransa.

Rais wa Zamani wa Ivory Coast President Laurent Gbagbo (Katikati) akiwa na mwanasheria wake Emmanuel Altit (Kulia)t for the start of the trial at the International Criminal Court in The Hague, Netherlands, January 28, 2016
Rais wa Zamani wa Ivory Coast President Laurent Gbagbo (Katikati) akiwa na mwanasheria wake Emmanuel Altit (Kulia)t for the start of the trial at the International Criminal Court in The Hague, Netherlands, January 28, 2016 REUTERS/Peter Dejong/Pool
Matangazo ya kibiashara

Katika maelezo yao ya awali kwenye mahakama ya ICC ikiwa ni siku ya tatu toka kuanza kwa kesi dhidi ya kiongozi huyo, ambapo wakili wake, Emmanuel Altit ameileza mahakama namna ambavyo Ufaransa ilimsaidia Ouattara kuchukua madaraka kwa nguvu.

Wakili Altit, ameongeza kuwa, rais Ouattara na wafuasi wake, walitaka kuchukua madaraka kwa nguvu ikiwa ni pamoja na kugombea mji wa Abidjan, ilikuwa ni wazi kabisa kuwa mpango wake ulipangwa kwa kusaidiwa na Ufaransa.

Rais wa zamani wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo akiwa kwenye mahakama ya ICC mjini The Haguerimes contre l'humanité, au premier jour de son procès devant la CPI, jeudi 28 janvier 2016.
Rais wa zamani wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo akiwa kwenye mahakama ya ICC mjini The Haguerimes contre l'humanité, au premier jour de son procès devant la CPI, jeudi 28 janvier 2016. REUTERS/Peter Dejong

Gbagbo na mtuhumiwa mwingine, Charles Ble Goude, kiongozi wa kundi la vijana lililokuwa linamuunga mkono, wamekana mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu baada ya watu elfu 3 kuuawa wakati wa vurugu za mara baada ya uchaguzi mkuu wa 2010.

Kesi hii ya aina yake ambayo ni ya kwanza kushuhudia rais wa zamani akisimama kizimbani, inatarajiwa kudumu kwa zaidi ya miaka mitatu.

Gbagbo alijitangaza kuwa mshindi wa uchaguzi wa mwaka 2010, lakini mataifa yenye nguvu duniani ikiwemo Marekani na Ufaransa pamoja na umoja wa Mataifa walimuunga mkono Ouattara aliyeshinda kwa idadi ndogo ya kura.

Mawakili wa Gbagbo wamewaambia majaji wa mahakama ya ICC, kuwamteja wao ametengenezewa kesi, kesi ambayo wahusika wake ni taifa la Ufaransa, ambalo lilihakikisha Ouattara anaingia madarakani kwa nguvu.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.