Pata taarifa kuu

Jengo la Westgate latazamiwa kuanza shughuli zake

Nchini Kenya, Jengo la kibiashara la Westgate jijini Nairobi lilivamiwa na wanamgamabo wa Al Shabab kutoka nchini Somalia mwaka 2013 na kuwauwa watu zaidi ya 60 litafunguliwa tena mwezi Julai mwaka huu.

Jengo la kibiashara la Westgate lililovamiwa na wanamgambo wa Al Shabab mwaka 2013 na kuwaua watu zaidi ya 60, jijini Nairobi., Nairobi, Kenya, le 23 septembre 2013.
Jengo la kibiashara la Westgate lililovamiwa na wanamgambo wa Al Shabab mwaka 2013 na kuwaua watu zaidi ya 60, jijini Nairobi., Nairobi, Kenya, le 23 septembre 2013. REUTERS/Johnson Mugo
Matangazo ya kibiashara

Tangu kutokea kwa shambulizi hilo, jengo hilo lilifungwa ili kukarabatiwa upya.

Mbali na maafisa, shambulizi hilo lilisababisha hasara ya Mamilioni ya fedha kwa wafanyibishara waliokuwa wamewekeza katika jengo hilo.

Wasimamizi wa jengo hilo pamoja na wafanyibiashara walikutana Jumanne wiki hii jijini Nairobi wakati wa maombi ya kidini kwa maandalizi ya ufunguzi wa jengo hilo.

Hayo yakijiri wasichana wawili, Salwa Abdalla na Tawfiqa Dahir ambao marafiki wametoweka kutoka nyumbani kwao mjini Nairobi nchini Kenya.
Wasichana hao wanashukiwa kusafiri nchini Syria ili kujiunga na kundi la wapiganaji wa ISIS.

Awali wasichana hao walisikika wakidai kwamba walikuwa wakielekea katika shule moja ya kiislamu lakini sasa wametoweka.

Familia za Salwa Abdalla na Tawfiqa Dahir zimesema kuwa zilipokea ujumbe kutoka kwa mmoja wa wasichana hao akisema kuwa wako nchini Syria.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.