Moscow-Cairo: Ushirikiano waendelea kupiga hatua maridhwa
Rais wa Misri Abdel Fattah Al-Sissi yuko katika ziara rasmi aliyoibuni jana nchini urusi, hii ikiwa ndio ziara yake ya kwanza nchini humo tangu kushika hatamu za uongozi wa Misri.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Rais Sissi alionyeshwa vifaa kadhaa vya kijeshi vilivyokuwa vimewekwa katika uwanja wa ndege mjini Sochi kwa ajili ya kuvikaguwa mara alipowasili mjini Moscow nchini Urusi, Vifaa hivyo vya kijeshi ni pamoja na magari mapya ya deraya na mifumo ya makombora.
Katika mazungumzo yake na wanahabari punde baada ya kukutana na raisi Vladmiri Putin wa Urusi, Sissi amesema amepigwa na butwaa na kuridhika na ushirikiano wa Urusi.
Urusi kupitia ushirikiano uliopanuliwa wa kijeshi na kiuchumi , imepata nafasi kubwa ya ushawishi nchini Misri, ambayo ni mshirika muhimu wa Marekani katika mashariki ya kati.
Katika kipindi cha miezi sita pekee mwaka 2014 watali nusu milioni kutoka nchini Urusi wameingia nchini Misri. Lakini rais wa Misri, Abdel Fattah Al-Sissi anataka Urusi iwekeze katika sekta ya viwanda na mafuta.
Misri inataka pia makampuni ya gesi ya Urusi yaanzishe zoezi la kuchimba mafuta na gesi, ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa taifa hilo, katika bahari ya Mediterania. Viongozi hao wawili wamezungumzia pia ushirikiano katika masuala ya nuklia.