Pata taarifa kuu
SUDANI KUSINI-Uhuru-Siasa

Sudani Kusini yaadhimisha miaka mitatu ya uhuru

Nchi ya Sudan kusini ambayo ni taifa changa duniani inasherehekea hii leo miaka mitatu ya uhuru wake katika muktadha wa vita vya wenyewe kwa wenyewe, baada ya miezi kadhaa ya mauaji ya kikabila. Tifa hilo pia linakabiliwa na kitisho cha njaa.

Rais wa Sudani Kusini, Salva Kiir akiambatana na rais wa Siudani, Omar el-Béchir wakisabahi umati katika sherehe za uhuru, Julai 9 mwaka 2011.
Rais wa Sudani Kusini, Salva Kiir akiambatana na rais wa Siudani, Omar el-Béchir wakisabahi umati katika sherehe za uhuru, Julai 9 mwaka 2011. REUTERS/Goran Tomasevic
Matangazo ya kibiashara

Vita hivyo ambavyo vinavyotokana na malumbano kati ya rais Salva Kiir na aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar vimesababisha watu wasiopungua milioni moja na nusu kuyakimbia makazi yao na mamia kwa maelfu kuuwawa.

Gwaride la wanajeshi wa Sudani Kusini wakijiandaliwa sherehe za kupata uhuru, Julai 5 mwaka 2014.
Gwaride la wanajeshi wa Sudani Kusini wakijiandaliwa sherehe za kupata uhuru, Julai 5 mwaka 2014. REUTERS/Goran Tomasevic

Raia wa Sudan Kusini "ni waathirika wa kwanza wa vita hivyo ambavyo kwa mujibu wa wadadisi vinaiathiri nchi hiyo katika nyanja zote.

Sudani Kusini ilipata uhuru wake Julai 9 mwaka 2011, baada ya kujitenga na khartoum.

Hata hivo taifa la Sudani Kusini linakabiliwa na baa la njaa. Hayo yanathibitishwa na shirika la kihisani la Oxfam.

“Sudani Kusini inakabiliwa wakati huu na tatizo kubwa, ambapo watu takriban milioni 4 sawa na theluthi moja ya raia wake wanakabiliwa na baa la nja, huku msaada unaotolewa kwa walengwa ukiwa hautoshi, limesema shirika hilo la Oxfam, likibaini kwamba nusu ya watu hao ndio wananufaika na msaada huo.

Katika maeneo kadhaa hususan Jonglei (mashariki), jamii za wafugaji wamepoteza mifugo yao, huku wakulima wakiwa hawana mbegu wakati zinasalia siku chache ili msimu wa kulima ufikiye ukingoni.

Raia wa Sudani Kusini wakipewa hifadhi katika kambi iliyojengwa kwenye maeneo kunakopatikana ofisi za Umoja wa Mataifa.
Raia wa Sudani Kusini wakipewa hifadhi katika kambi iliyojengwa kwenye maeneo kunakopatikana ofisi za Umoja wa Mataifa. Reuters/路透社

Njaa hio imesababisha takriban watu 100.000 wanayahama makaazi yao na kuomba hifadhi kwenye ofisi za Umoja wa Mataifa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.