Pata taarifa kuu
WHO-AFRIKA-Afya

WHO yatiwa wasiwasi na kusambaa kwa virusi vya Ebola Afrika

Shirika la afya duniani WHO linasema kuwa idadi ya watu waliokufa kutokana na virusi vya ugonjwa wa Ebola kwenye nchi za Afrika Magharibi imefikia watu 467 na kuonya kuwa idadi hiyo huenda ikaongezeka.

Madaktari wa Shirika la Madaktari wasio na Mipaka MSF wanabeba muili wa mtu aliefariki kutokana na ugonjwa wa Ebola katika mji wa Guékédou, nchini Guinea, Aprili 01 mwaka 2014.
Madaktari wa Shirika la Madaktari wasio na Mipaka MSF wanabeba muili wa mtu aliefariki kutokana na ugonjwa wa Ebola katika mji wa Guékédou, nchini Guinea, Aprili 01 mwaka 2014. AFP PHOTO / SEYLLOU
Matangazo ya kibiashara

Mwanasayansi akifanya utafiti juu ya  virusi vya Ebola.
Mwanasayansi akifanya utafiti juu ya virusi vya Ebola. Tyler Hicks/Liaison

Kwenye taarifa yake kwa vyombo vya habari kuhusu mwenendo wa ugonjwa huo uliozikumba nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone, WHO inasema kuwa mpaka sasa wamebaini kuwepo kwa maambukizi mapya zaidi ya watu 759 kwenye ukanda huo hali inayoogofya kuhusu kuendelea kusambaa kwa virusi hivyo.

Idadi hii mpya inafanya kufikia kiwango cha asilimia 38 cha maambukizi mapya ukilinganisha na kiwango cha asilimia 27 mwezi Aprili mwaka huu wakati Shirika la Afya Duniani lilipotoa takwimu za mwisho kuonesha mwenendo wa ugonjwa huo ambao ulionekana kana kwamba umedhibitiwa.

Virusi vya Ebola.
Virusi vya Ebola. CDC/ Cynthia Goldsmith

Takwimu hizi zimetolewa wakati wa mkutano unaowakutanisha mawaziri wa afya toka mataifa kumi na moja ya ukanda wa Afrika Magharibi, mkutano unaofanyika nchini Ghana ukilenga kutafuta mbinu mpya za kukabiliana na maambukizi zaidi ya virusi vya Ebola.

Nyama za wanyama pori, hususan popo, nyani, zimekua zikiuzwa kando na barabara za mji wa Yamoussoukro, nchini Côte d'Ivoire. Wanasayansi wana mashaka kuwa baadhi ya wanyama nachangia virusi vya  Ebola kusambaa.
Nyama za wanyama pori, hususan popo, nyani, zimekua zikiuzwa kando na barabara za mji wa Yamoussoukro, nchini Côte d'Ivoire. Wanasayansi wana mashaka kuwa baadhi ya wanyama nachangia virusi vya Ebola kusambaa. REUTERS/Thierry Gouegnon

Virusi vya Ugonjwa wa Ebola huweza kuambukizwa kwa njia ya hewa na kugusana hii ni kwa mujibu wa ripoti ya WHO, ambapo umetajwa kuwa miongoni mwa magonjwa hatari zaidi duniani, ugonjwa ambao mpaka sasa haujapatiwa tiba.

Mtu aupatapo ugonjwa huu huweza kuwa na homa kali, maumivu ya viungo, kutapika na kuhara na wakati mwingine kushindwa kufanya kazi kwa baadhi ya ogani za mwili na kutokwa damu mfululizo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.