Watatu wajeruhiwa katika shambulizi la guruneti mjini Garissa Kenya
Watu watatu wamejeruhiwa katika shambulizi la guruneti katika mji wa Garisa nchini Kenya jana Jumamosi mkuu wa polisi wa eneo hilo amethibitisha.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Kati ya vijana wawili au watatu wanadaiwa kurusha guruneti hilo ndani ya karakana na kujeruhi mafundi makenika watatu, kabla yakukimbia ameeleza mkuu wa polisi katika kaunti ya Garissa Charles Kinyua.
Hata hivyo sababu za kufanya shambulio katika eneo hilo jirani na mpaka wa Somalia hazikujulikana.
Kenya imekuwa ikikumbwa na mashambulizi ya maguruneti na bunduki ambayo mara kwa mara yanadaiwa kutekelezwa na waasi wa kiislam wa kundi la Al Shabab na mara kwa mara yamekuwa yakilemga idara za usalama kama polisi , tangu nchi hiyo ipeleke wanajeshi wake nchini Somalia kupambana na Al Shabab chini ya kikosi cha Umoja wa Afrika kinacholinda amani nchini Somalia AMISOM