Wanajeshi 6 wa FARDC wauawa mashariki mwa DRC
Wanajeshi sita wa jeshi la serikali, FARDC waliuawa katika shambulizi liliyotekelezwa na wapiganaji wa mai mai wa Kundi la APCLS dhidi ya ngome ya jeshi hilo katika mji wa Nyabondo,mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, taarifa kutoka Umoja wa Mataifa, MONUSCO zimethibitisha.
Imechapishwa:
Mashambulizi hayo yamefanywa na kundi linalofahamika kama muungano wa ukombozi wa Kongo huru, APCLS, katika eneo la Nyabyondo umbali wa kilomita 70 kaskazini mwa Goma katika mtaa wa Masisi, jimboni Kivu Kaskazini.
Le 30 avril 2014, le groupe APCLS a attaqué le poste opérationnel MONUSCO et les positions des FARDC, situées à Birere 1 et Kishonga.
— MONUSCO (@MONUSCO) April 30, 2014
Msemaji wa jeshi la Umoja wa mataifa MONUSCO, Felix Prosper Baase, amewaambia waandishi wa habari katika mkutano wa Jumatano jana mjini Kinshasa kwamba mmoja wa wanajeshi wake pamoja na wanajeshi wengine walijeruhiwa katika tukio hilo.
Aidha ameeleza wanajeshi hao na wale wa serikali wamefanikiwa kudhibiti upya ngome yao hiyo huko Kivu Kaskazini.
Wakati huo huo serikali ya Kinshasa imetangaza orodha nyingine ya watu mia moja ambao wamepewa msamaha na rais Joseph Kabila akiwemo mbunge Muhindo Nzangi Bitondo aliyehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kumtusi Rais mwaka uliopita.
Hata hivyo, serikali ya DRC inawataka wananchi kutohatarisha usalama wa watu hao waliosamehewa au kuwanyanayapaa.